Nifanyeje?
- Zipi sifa za kuorodheshwa kama msaidizi wa mtaalam wa mifugo? (Enlisted Paraprofessional Assistant)
- Zipi sifa za kujiandikisha kama mtaalam msaidizi wa mifugo? (Enrolled Paraprofessional).
- Daktari wa mifugo asiye mtanzania (Foreigner) anasajiliwa vipi na Baraza.
- Daktari wa mifugo asiye Mtanzania anaweza kusajiliwa na kufanyakazi hapa nchini? (Temporary and permanent registration)?
MAAFISA UGANI WATAKIWA KUHAMASISHA “GESTI ZA MIFUGO” KATIKA MAENEO YAO

MAAFISA UGANI WATAKIWA KUHAMASISHA “GESTI ZA MIFUGO” KATIKA MAENEO YAO
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amewataka Maafisa Ugani kuhamasisha Gesti za mifugo kwa Wafugaji waliopo katika maeneo yao ikiwa ni moja ya hatua za kuhamasisha ufugaji wa kisasa hapa nchini.
Waziri Ulega ametoa maelekezo hayo wakati akifungua mafunzo rejea ya maafisa ugani 1000 wa nchi nzima yaliofanyika mjini Kibaha mkoani Pwani Machi 18, 2024.
“Washawishini watu wenye mashamba makubwa waliopo katika maeneo yenu waanzishe programu hii ya gesti za mifugo, tengenezeni mkakati mzuri wa kuhamasisha watu kufanya ufugaji wa kisasa kupitia gesti hizo za mifugo”, alisema