Pichani ni sehemu ya pikipiki 381 zilizotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa Maafisa Ugani nchini kwenye hafla fupi iliyofanyika Disemba 04,2025 jijini Dar-es-Salaam.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kushoto) akimkabidhi moja ya pikipiki 381 za Maafisa Ugani nchi nzima (wawakilishi waliokaa kwenye pikipiki) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe kwenye hafla fupi iliyofanyika Disemba 04,2025 jijini Dar-es-Salaam. Anayeshuhudia (nyuma) ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena akimkabidhi Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa nyaraka za utendaji wa ofisi yake Muda mfupi baada ya kuwasili Makao makuu ya Wizara hiyo yaliyopo eneo la Mtumba jijini Dodoma Novemba 18,2025.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akikagua moja ya chanjo za Mifugo mara baada ya kufika kwenye banda la Wakala ya Maabara ya Veterinari nchini (TVLA) wakati wa kilele cha Maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Chakula Duniani Oktoba 16,2025 mkoani Tanga. Kulia anayemuelezea ni Meneja wa Wakala hiyo mkoani humo Dkt. Olivia Manangwa.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiangalia moja ya pakiti za dagaa waliokaushwa kwa teknolojia ya Jua muda mfupi baada ya kufika kwenye banda la Wajasiriamali wa zao hilo wakati wa kilele cha Maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Chakula Duniani yaliyokuwa yakifanyika mkoani Tanga.
Msimamizi wa Dawati la lishe na Usalama wa Chakula kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Beatrice Mwijage akikabidhi mayai kwa mwakilishi wa wanafunzi wa shule ya Msingi Chuda iliyopo mkoani Tanga kwa lengo la kuhamasisha ulaji wa zao hilo la Mifugo kwa wanafunzi muda mfupi baada ya kufika shuleni hapo Oktoba 13,2025.