Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, akikagua kwa karibu miundombinu mbalimbali ya mradi wa Bandari ya Kilwa Masako, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao umefikia asilimia 98.9 ya ukamilishaji, Juni 06, 2026, Kilwa mkoani Lindi.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi (wa pili kutoka kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Agnes Meena (kushoto), Naibu Katibu Mkuu (Mifugo) Dkt. Fabian Madele (kulia) na Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh (wa pili kutoka kulia) wakiwa kwenye picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kusomwa kwa hotuba ya bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2026/2027, Mei 14,2026 Bungeni jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh akimueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan sifa za meli ya kwanza ya Uvuvi wa Bahari kuu aliyoizindua leo Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kushoto) akimueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan sifa za meli ya kwanza ya Uvuvi wa Bahari kuu aliyoizindua leo Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa Meli ya kwanza ya Uvuvi wa Bahari kuu uliofanyika leo Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa makao makuu ya Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam.
Nchi ya Qatar imefungua soko la nyama ya Mbuzi na Kondoo kutoka Tanzania ambalo ililifunga Agosti 25,2025 baada ya kupata taarifa ya uwepo wa ugonjwa wa midomo na miguu (FMD).