Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika (kulia katikati) akitoa chanjo ya mdondo wa kuku wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua utekelezaji wa kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo iliyofanyika Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Machi 16,2026. Kushoto kwake ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika (katikati) akimvalisha ng’ombe hereni ya utambuzi wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua utekelezaji wa kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo iliyofanyika Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Machi 16,2026.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Mhe. Joel Nanauka na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani (nyuma) wakiwakabidhi vijana waliohitimu programu ya Jenga kesho iliyo bora upande wa sekta ya Uvuvi (BBT-UVUVI) mfano wa hundi ya shilingi Bil.7 zilizotolewa kwenye hafla iliyofanyika leo Machi 07,2026 jijini Mwanza.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kulia) akikagua Mitamba inayozalishwa katika shamba la kuzalishia mifugo la Mabuki wakati wa Ziara yake Januari 24, 2026 Mabuki, Mkoani Mwanza.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Wa kwanza, kushoto) akizungumza Ujumbe wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) nchini Tanzania kujadili miradi inayotekelezwa katika sekta ya mifugo na uvuvi, wakati wa Kikao kilichofanyika ofisini kwake Januari 16, 2026 Mtumba, Jijini Dodoma.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akiwalisha chakula samaki kwenye moja ya mabwawa yaliyopo kwenye kituo cha ukuzaji Viumbe Maji cha Rubambagwe kilichopo Chato mkoani Geita Januari 05,2026.