Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh akimueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan sifa za meli ya kwanza ya Uvuvi wa Bahari kuu aliyoizindua leo Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kushoto) akimueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan sifa za meli ya kwanza ya Uvuvi wa Bahari kuu aliyoizindua leo Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa Meli ya kwanza ya Uvuvi wa Bahari kuu uliofanyika leo Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa makao makuu ya Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam.
Nchi ya Qatar imefungua soko la nyama ya Mbuzi na Kondoo kutoka Tanzania ambalo ililifunga Agosti 25,2025 baada ya kupata taarifa ya uwepo wa ugonjwa wa midomo na miguu (FMD).
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika (kulia katikati) akitoa chanjo ya mdondo wa kuku wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua utekelezaji wa kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo iliyofanyika Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Machi 16,2026. Kushoto kwake ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika (katikati) akimvalisha ng’ombe hereni ya utambuzi wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua utekelezaji wa kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo iliyofanyika Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Machi 16,2026.