Pichani ni muonekano wa sasa wa Bandari ya kisasa ya Uvuvi iliyojengwa na Serikali ya awamu ya 6 Wilayani Kilwa Masoko mkoa wa Lindi.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack (aliyekaa kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena (aliyekaa kushoto) na watendaji mbalimbali wa Wizara wakishuhudia namna kamera za ulinzi zinavyofanya kazi wakati wa zoezi la kujaribu mitambo mbalimbali ya bandari ya Uvuvi iliyopo Kilwa Masoko mkoani humo inavyofanya kazi Juni 26,2026.
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo (DGLF), Dkt. Asimwe Rwiguza (wa pili kulia), akimuonesha na kumuelezea Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (wa pili kushoto), Malisho ya aina mbalimbali ambayo yanatumika kulisha Mifugo, katika Uzinduzi wa Maonesho na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 19, 2026, Chalinze - Pwani, wa tatu kushoto ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, akikagua kwa karibu miundombinu mbalimbali ya mradi wa Bandari ya Kilwa Masako, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao umefikia asilimia 98.9 ya ukamilishaji, Juni 06, 2026, Kilwa mkoani Lindi.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi (wa pili kutoka kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Agnes Meena (kushoto), Naibu Katibu Mkuu (Mifugo) Dkt. Fabian Madele (kulia) na Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh (wa pili kutoka kulia) wakiwa kwenye picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kusomwa kwa hotuba ya bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2026/2027, Mei 14,2026 Bungeni jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh akimueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan sifa za meli ya kwanza ya Uvuvi wa Bahari kuu aliyoizindua leo Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam.