Nifanyeje?
- Zipi sifa za kuorodheshwa kama msaidizi wa mtaalam wa mifugo? (Enlisted Paraprofessional Assistant)
- Zipi sifa za kujiandikisha kama mtaalam msaidizi wa mifugo? (Enrolled Paraprofessional).
- Daktari wa mifugo asiye mtanzania (Foreigner) anasajiliwa vipi na Baraza.
- Daktari wa mifugo asiye Mtanzania anaweza kusajiliwa na kufanyakazi hapa nchini? (Temporary and permanent registration)?
TARATIBU ZA KUSAFIRISHA MIFUGO NDANI NA NJE YA NCHI
1. KUTOKA KWA WATU BINAFSI
Nyaraka muhimu wakati wa kusafirisha Mifugo kutoka kwa mtu binafsi:- Uthibitiso/Kibali cha uhalali wa Umiliki wa Mifugo Kibali cha hali ya Afya ya Mifugo (Livestock Health Certificate) Kibali cha kusafirishia Mifugo (Livestock Movement Permit).
2. KUTOKA KATIKA MINADA YA MIFUGO
Nyaraka muhimu wakati wa kusafirisha Mifugo kutoka Minada ya Mifugo:-
Leseni ya kufanya biashara ya mifugo ndani au nje ya nchi;
Malipo ya Ushuru wa Mnadani (Market fee);
Cheti cha hali ya Afya ya Mifugo (Livestock Health Certificate) Kibali cha kusafirishia Mifugo (Livestock Movement Permit).
3. KWENDA NJE YA NCHI
Nyaraka muhimu wakati wa kusafirisha Mifugo kutoka kwenda nje ya Nchi:-
Leseni ya kufanya biashara ya Mifugo nje ya nchi;
Kibali cha ruhusa ya kuingiza mifugo kwenye nchi inapopelekwa mifugo (importation permit);
Kibali cha Hali ya Afya ya Mifugo (Livestock Health Certificate); Uthibitisho wa Malipo ya Ushuru wa Mnadani (Market fee);
Uthibitisho wa Malipo ya ushuru wa kusafirisha Mifugo nje ya nchi (Exportation Fee)
Kibali cha Kusafirisha Mifugo nje ya nchi (Export permit)