WIZARA YAWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MIRADI KWA KAMATI

Imewekwa: Monday 13, March 2023

Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo na kuwasilisha taarifa ya muundo na majukumu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, taarifa ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa Bwawa la kuvuna maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo la Matekwe lililopo Nachingwea, Mkoani Lindi, na taarifa ya ujenzi wa bandari ya uvuvi iliyopo Wilayani Kilwa, Mkoani Lindi.

Baada ya kupokea taarifa hiyo mapema leo Machi 12, 2023, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. David Kihenzile alimuhakikishia Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega kuwa watashirikiana bega kwa bega na Wizara ili kuiwezesha kufikia malengo yake ya kuwahudumia wananchi ili wapate maendeleo katika shughuli zao za kila siku za ufugaji na uvuvi.

Aidha, kamati hiyo inatarajiwa kufanya ziara Mkoani Lindi hivi karibuni kwa ajili ya kutembelea na kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo.

.