Nifanyeje?
- Zipi sifa za kuorodheshwa kama msaidizi wa mtaalam wa mifugo? (Enlisted Paraprofessional Assistant)
- Zipi sifa za kujiandikisha kama mtaalam msaidizi wa mifugo? (Enrolled Paraprofessional).
- Daktari wa mifugo asiye mtanzania (Foreigner) anasajiliwa vipi na Baraza.
- Daktari wa mifugo asiye Mtanzania anaweza kusajiliwa na kufanyakazi hapa nchini? (Temporary and permanent registration)?
USHIRIKIANO WA BODI YA MAZIWA NA SEKTA BINAFSI KUONGEZA USINDIKAJI WA MAZIWA HAPA NCHINI

Bodi ya Maziwa yasisitiza ushirikiano na sekta binafsi katika kuongeza usindikaji wa maziwa nchini.
Hayo yamesemwa na Msajili wa Bodi ya Maziwa, Bw. Noely Byamungu wakati wa kikao kazi cha kubainisha maeneo ya ushirikishwaji na Sekta Binafsi kilichofanyika jana (20.11.2020) jijini Dar es Salaam.
Kikao kazi hicho kililenga kupitia Mpango Mkakati wa miaka mitano 2020/21-2025/26 wa Bodi ya Maziwa na kubainisha namna ya bora ya ushirikishwaji wa sekta binafsi katika utekelezaji wa majukumu ya Bodi.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda na Makampuni ya Wasindikaji Maziwa ya UHT nchini kutoka kampuni ya Asas Dairies, Tanga Fresh, Milkcom na Azam Dairies, Wabia wa maendeleo kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Mradi wa Wasindikaji wa Maziwa Tanzania (TMPP).
Bw. Byamungu alisema kuwa lengo la Bodi ya Maziwa ni kuwezesha viwanda kuongeza uwezo wa kusindika maziwa ambao kwa sasa usindikaji wa maziwa katika viwanda hivyo ni asilimia 23.52.
Aidha, Msajili amesema kuwa Bodi ya Maziwa ipo tayari kuunga mkono jitihada za wadau wa Tasnia ya Maziwa kufikia malengo yao ya kuzalisha maziwa kwa kiwango kilichosimikwa.
Bw. Byamungu alisema kuwa kikao hicho kitaleta mtazamo wa muda mrefu wa Tasnia ya maziwa katika usindikaji na kutoa ramani ya kuongezeka kwa ushirikishwaji wa wadau, mawasiliano na ushirikiano miongoni mwa sekta binafsi, wabia wa maendeleo na wadau wengine kwenye sekta.
"Bodi ya Maziwa iko tayari na ina nia njema ya kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya kuwa sekta endelevu katika uzalishaji, usindikaji na masoko ya maziwa na bidhaa zake nchini" Alisema Bw. Byamungu.
Nae Mkurugenzi wa Mradi wa Wasindikaji Tanzania, Bw. Mark Tsoxo amesema wapo tayari kuisaidia Bodi ya Maziwa kutekeleza majukumu yake ya kuongeza usindikaji wa maziwa nchini ili kuimarisha mnyororo mzima wa thamani. Pia ameiomba Bodi ya Maziwa kuendelea kushirikiana na Sekta Binafsi kwa Ukaribu ili kufikia azma iyo.
Tasnia ya Maziwa ina mchango mkubwa katika kuhakikisha usalama wa chakula na kupunguza umaskini.