Nifanyeje?
- Zipi sifa za kuorodheshwa kama msaidizi wa mtaalam wa mifugo? (Enlisted Paraprofessional Assistant)
- Zipi sifa za kujiandikisha kama mtaalam msaidizi wa mifugo? (Enrolled Paraprofessional).
- Daktari wa mifugo asiye mtanzania (Foreigner) anasajiliwa vipi na Baraza.
- Daktari wa mifugo asiye Mtanzania anaweza kusajiliwa na kufanyakazi hapa nchini? (Temporary and permanent registration)?
PROF. SHEMDOE AKUTANA NA MWAKILISHI MKAAZI WA SHIRIKA LA JICA
![](https://www.mifugouvuvi.go.tz/uploads/news/medium-1707387153-IMG-20240208-WA0005.jpg)
PROF. SHEMDOE AKUTANA NA MWAKILISHI MKAAZI WA SHIRIKA LA JICA
Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe amekutana na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Ara Hitoshi kujadiliana utekelezaji wa makubaliano ya kuendeleza mradi wa Afya Moja unaoangalia magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwenye Mifugo kwenda kwa binadamu ikiwepo Brucellosis na Kifua Kikuu (TB).
Prof. Shemdoe amekutana na Mwakilishi huyo Ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma Januari 7, 2024.
Mradi huo unasimamiwa na Wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Maprofesa kutoka Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Maprofesa kutoka Chuo cha Mifugo cha Rakuna, kilichopo katika Mji wa Hokaido nchini Japan.