Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Mifugo na Uvuvi

DKT. BASHIRU AZIAGIZA LITA, TARILI KUFANYA MAGEUZI SEKTA YA MIFUGO

Imewekwa: 28 January, 2026
DKT. BASHIRU AZIAGIZA LITA, TARILI KUFANYA MAGEUZI SEKTA YA MIFUGO

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ameitaka Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA) na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kutumia mafunzo na tafiti za mifugo za kisasa  kuwanufaisha wafugaji nchini.

Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ametoa agizo hilo leo Januari 24, 2026 wakati wa ziara yake kwenye taasisi hizo zilizopo Mabuki mkoani Mwanza, ambapo amesema tafiti na mafunzo  ya mifugo yanayoendana na wakati yatumike kuwabadilisha wafugaji kufuga kisasa.

“Utafiti wetu mzuri, mafunzo yetu mazuri vitumike kwenda kubadilisha wafugaji, sisi tuwachague wale ambao wameshabadilika na wamewekeza , tuwape utaalam zaidi ili watumike kama wasambazaji wa teknolojia” alisema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.

Aidha, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru aliitaka LITA kufanya ufuatiliaji wa utaalam unaotolewa kwa wafugaji kutokana na mafunzo yanayotolewa na Wakala huo huku TALIRI ikiagizwa kufuatilia matumizi ya tafiti kutoka kwa wadau wa sekta ya mifugo.

Katika hatua nyingine alihimiza wataalam kuzingatia maadili ya taaluma katika kuwahudumia wafugaji ili kuimarisha ushirikiano utakaokuza sekta ya mifugo nchini.

Mrejesho, Malalamiko au Wazo