Nifanyeje?
- Zipi sifa za kuorodheshwa kama msaidizi wa mtaalam wa mifugo? (Enlisted Paraprofessional Assistant)
- Zipi sifa za kujiandikisha kama mtaalam msaidizi wa mifugo? (Enrolled Paraprofessional).
- Daktari wa mifugo asiye mtanzania (Foreigner) anasajiliwa vipi na Baraza.
- Daktari wa mifugo asiye Mtanzania anaweza kusajiliwa na kufanyakazi hapa nchini? (Temporary and permanent registration)?
SHEMDOE ABAINISHA FURSA ZA MALISHO YA MIFUGO

Na. Omary Mtamike
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe amewataka wafugaji nchini kuendelea kutenga maeneo ya kuzalisha malisho ya mifugo yao ili waendelee kuboresha afya za wanyama na kujipatia kipato baada ya kuyauza.
Prof. Shemdoe amesema hayo Aprili 14,2025 wakati akifungua kikao cha wataalam wa malisho ya Mifugo kilichofanyika mkoani Morogoro ambapo ametoa rai kwa vijana kuchangamkia fursa hiyo kama wanavyofanya kwenye shughuli nyingine za kiuchumi.
“Tuwawezeshe vijana waanzishe mashamba ya kulima malisho kwa sababu nina uhakika masoko yapo na nina mfano wa mtu mmoja hapa Pwani yeye kila mwaka anauza tani nyingi za malisho na hana biashara nyingine zaidi ya hiyo” Ameongeza Prof. Shemdoe.
Aidha katika hatua ya utekelezaji wa maazimio ya kikao kilichopita cha wataalam hao, Prof. Shemdoe amesema Wizara yake imeendelea kuajiri vijana wengi wanaotokana na shahada ya nyanda za malisho huku pia wakiendelea kutoa elimu kuhusu chakula stahiki kwa mifugo.
Akizungumza awali kabla ya kumkaribisha Prof. Shemdoe, Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Ismail Selemani ameishukuru Wizara kwa kufanyia kazi baadhi ya maazimio ya wataalam hao ikiwa ni pamoja na kuboresha sheria ya Maeneo ya Malisho na rasilimali za vyakula vya Mifugo namba 180 ya mwaka 2010 na kuendelea kutenga maeneo ya malisho na uanzishwaji wa mashamba darasa ya malisho hayo.
Akigusia fursa inayotokana na malisho Visiwani Zanzibar, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo visiwani humo Dkt. Abdultwalib Suleiman amesema kuwa wafugaji waliopo huko wamekuwa na changamoto ya uzalishaji wa malisho kutokana na sehemu kubwa ya visiwa hivyo kuzungukwa na majengo na miundombinu mbalimbali hivyo amewataka wazalishaji wa malisho ya Mifugo kuzalisha malisho ya kutosha na kuyapeleka Zanzibar.