Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (kulia) akimkabidhi tuzo mwandishi wa habari kutoka gazeti la Uhuru Bw. Musa. Musa baada ya kuibuka kinara wa uandishi wa habari zinazohusu sekta za Mifugo na Uvuvi kwenye hafla iliyofanyika Mei 05, 2025 jijini Dar es Salaam.
Pichani ni jengo la hosteli ya Wasichana la “Dkt. Ashatu Kijaji” lililopo kwenye Wakala ya Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) kampasi ya Mpwapwa ambalo limezinduliwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji Mei 08, 2025 Mpwapwa, Dodoma.
Ndege nyuki (drone) yenye namba za usajili 5H-25038 kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), ambayo ni maalum kwa ajili ya kudhibiti uvuvi haramu ikiwa angani kwa mara ya kwanza baada ya kuzinduliwa rasmi Aprili 13, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikabidhi Vyeti kwa mnufaika wa Mradi wa pili wa ukopeshaji Boti za Kisasa wakati wa Uzinduzi wa Mradi huo mkoani Tanga Februari 26, 2025.
Serikali imewawezesha wanawake wanaojishughulisha na Uvuvi mitaji ya kuendeleza shughuli zao
Zao la Mwani mbali na bidhaa zake kuwa na manufaa kwenye afya ya mtumiaji limekuwa mkombozi wa kiuchumi kwa wakulima waliopo ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi.