Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Agness Meena (kulia kwake) na baadhi ya Wakurugenzi na watendaji wa Wizara hiyo Agosti 08, 2025 muda mfupi baada ya Wizara hiyo kutangazwa vinara wa maonesho ya kimataifa ya Nane Nane mwaka 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kulia) akipokea maelezo kuhusu matumizi ya Ndege Nyuki kwenye udhibiti wa vitendo vya uvuvi haramu ndani ya ziwa Victoria muda mfupi baada ya kufika kwenye banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi ndani ya Viwanja vya Nnane Nane vya Dkt. John Samwel Malecela Agosti 08, 2025 jijini Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kulia) akimuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) Prof. Erick Komba (kushoto) kuhusu kuongeza kiwango cha uzalishaji wa mbari za Mifugo ili kuhamasisha ufugaji wa kisasa nchini muda mfupi baada ya kufika kwenye banda hilo Agosti 08, 2025 kwenye Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akitoa maelekezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agness Meena (kushoto kwake) kuhusu kutoa elimu ya ufugaji samaki kwa wananchi wote hasa wale wa kipato cha kati na chini alipofika kwenye eneo la Wizara hiyon Agosti 03,2025.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agness Meena akimueleza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango huduma zinazopatikana kwenye mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi muda mfupi baada ya Dkt. Mpango kuwasili hapo Agosti 1, 2025 ambako alitembelea Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) nw Shamba la kuzalisha Mifugo la Kitulo.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (katikati) akikabidhi zana za Uvuvi kwa wawakilishi wa vikundi vya mikoa ya Pwani na Dar-es-Salaam muda mfupi baada ya kuwakabidhi boti za kisasa za Uvuvi Julai 16, 2025 jijini Dar-es-Salaam.