Menejimenti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikifuatilia uwasilishwaji wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo iliyokuwa ikisomwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani) Mei 23, 2025, Bungeni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (kushoto), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya Mifugo Ndg. Abdul Mhinte (kulia) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya Uvuvi Dkt. Edwin Mhede (katikati) wakifuatilia hotuba ya Bajeti iliyokuwa ikisomwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani) Mei 23, 2025 jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Afisa Tehama kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Joseph Nkwabi wakati akiangalia namna mfumo wa utambuzi wa Mifugo kupitia hereni za kielektronoki unavyofanya kazi muda mfupi baada ya kuzindua kampeni ya Chanjo na utambuzi wa Mifugo kwenye viwanja vya Nyakabindi, Bariadi mkoani Simiyu Juni 16, 2025.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akisoma Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni jijini Dodoma Mei 23, 2025.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (kulia) akimkabidhi tuzo mwandishi wa habari kutoka gazeti la Uhuru Bw. Musa. Musa baada ya kuibuka kinara wa uandishi wa habari zinazohusu sekta za Mifugo na Uvuvi kwenye hafla iliyofanyika Mei 05, 2025 jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kulia) akifurahia jambo na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa hafla ya Uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya chanjo na utambuzi wa mifugo iliyofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi, Bariadi mkoani Simiyu Juni 16, 2025.