Menejimenti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikifuatilia uwasilishwaji wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo iliyokuwa ikisomwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani) Mei 23, 2025, Bungeni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (kushoto), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya Mifugo Ndg. Abdul Mhinte (kulia) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya Uvuvi Dkt. Edwin Mhede (katikati) wakifuatilia hotuba ya Bajeti iliyokuwa ikisomwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani) Mei 23, 2025 jijini Dodoma.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Alexander Mnyeti wakiteta jambo mara baada ya kuwasilisha hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni jijini Dodoma Mei 23, 2025.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akisoma Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni jijini Dodoma Mei 23, 2025.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (kulia) akimkabidhi tuzo mwandishi wa habari kutoka gazeti la Uhuru Bw. Musa. Musa baada ya kuibuka kinara wa uandishi wa habari zinazohusu sekta za Mifugo na Uvuvi kwenye hafla iliyofanyika Mei 05, 2025 jijini Dar es Salaam.
Pichani ni jengo la hosteli ya Wasichana la “Dkt. Ashatu Kijaji” lililopo kwenye Wakala ya Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) kampasi ya Mpwapwa ambalo limezinduliwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji Mei 08, 2025 Mpwapwa, Dodoma.